Saturday, July 11, 2009

LIBENEKE LA WIKIENDI BADO LINAENDELEA.....

Unadhani kwanini Waafrika hatuwezi kuwa Magaidi?
Sababu ni hizi hapa mdau.......................

1. Mara zote sisi ni wachelewaji:Inawezekana wote tukachelewa ndege.

2. Wahudumu warembo wa kwenye ndege wanaweza kuwa kikwazo kwetu kutimiza azma yetu.

3. Tunaongea kwa sauti sana na hivyo na kufanya kukosekana kwa usiri.

4. Vyakula na vinywaji ndani ya ndege vinaweza kutusahaulisha tunachotakiwa kukifanya.

5. Tunaongea kwa ishara hasa kwa kutumia mikono hali ambayo itatulazimu tuweke silaha chini wakatiwa shughuli nzima ya ugaidi.

6. Wote tunataka kupanda ndege.

7. Tutabishana na kuanza kupigana ndani ya ndege.

8. Hatuwezi kutunza siri: inawezeka wiki moja kabla ya tukio kila mtu akawa anajua nini kitafanyika.

9. Tutaweka bendera za nchi zetu katika vioo vya ndege.

10. Tunaweza kujikuta wote tunagombania kupigaji picha ambazo zitakuwa zikichukuliwa na mmoja kati ya mateka katika ndege husika.

No comments:

Post a Comment