Thursday, November 18, 2010

MDAU KUWA MAKINI SANA NA ULACHO KAMA IKATOKEA SIKU UMETEMBELEA KIJIJI CHA MADAMBA HUKO MSUMBIJI..


Hii ni safari ya baadhi ya wakazi wa kijiji cha Madamba nchini Msumbiji wakielekea porini si kuwinda wanyama ama kulima hapana hii ni safari inayohusisha kukamata panya ambao hutumika kama kitoweo na wengine wakiuzwa kando ya barabara kuu inayopita kijijini hapo.


Wakati panya huyu ameshaadhibiwa kazi ipo kwa mwingine ambaye anaonesha kila jitihada za kuokoa roho yake.

Amenasa huyu kiulaini kabisa hana ujanja.


Wakati mwingine inabidi kuchimba mashimo katika sehemu ambazo wawindaji huhisi kuwa huenda kukawa na Panya.

Kazi kama imeisha kwa mafanikio hivi maana kila muwindaji anaonekana akiwa na Panya wake.


Wakati mwingine moto hutumika katika kuwapata kirahisi Panya wa kitoweo na biashara.


Hapa sasa Panya wako katika maandalizi kabla ya kuchomwa vizuri kisha kupelekwa sokoni kwaajili ya kuuzwa kwa wanaohitaji kitoweo hicho.


Kitu cha Panya sasa kinachomwa.


Huku Mahindi ya kuchoma huku mishikaki ya Panya.


Biashara nzuri wateja ni wengi kweli kweli.


Mdau huyu akiwa anaikonga roho yake kwa kujipatia Panya kwa senti 30 tu za Msumbiji.


Panya kwa ugali mdau raha iliyoje....


Amini usiamini hawa ndio Panya ambao huku Tanzania tumekuwa tukitumia kila njia kuhakikisha kuwa hawaingii katika nyumba zetu kwa kuhofia uharibifu unaoweza kusababishwa na wanyama hao.






Rosti ya Panya ikiwa jikoni mdau....


Wachuuzi wa Panya wakiwa mapumzikoni baada ya purukushani za hapa na pale kugombea wateja.


Unaweza kujionea hapa mdau panya hao hutungwa katika kijiti wakiwa 6-7 hivi wakiwa wamechomwa vizuri kabisa na humgharimu mteja kiasi cha senti 30 za Msumbiji kuweza kujipatia kitoweo hicho.

Kila muwinda panya mwisho wa siku huambulia kiasi cha dola3 za kimarekani ambazo zinawasaidia kuongeza kipato katika familia zao.

3 comments:

  1. Ni wamakonde hawa....wanakula sna panya na huwa wanawapenda mno.

    ReplyDelete
  2. That is not true,just showing us to believe,These small animals can have
    a dangerous disease.

    ReplyDelete