Tuesday, June 4, 2013

NIMEFANYA KILA NALOTAKA KATIKA UJANA WANGU SASA NIMEAMUA KUTULIA NA HUYU!!.























Bondia Amir Khan akiwa na mke wake Faryal Makhdoom..



Amir Khan 26 mwishoni mwa wiki iliyopita amefunga ndoa na Faryal Makhdoom katika sherehe ya kimila iliyofanyika katika hoteli ya Waldolf Astoria huko jijini New York.

Maharusi hao walionekana wakiwa katika mavazi ya kiutamaduni ya Kihindi ambapo bondia huyo aliahidi kuachana na maisha ya matanuzi na kutenga muda wa kutosha kwa mke wake ambae ni mwanafunzi wa political science.

Bondia huyo ameliambia jarida la Hello ameishi maisha ya ujana,amefanya kila kitu alichokuwa anakitaka kukifanya lakini sasa ameamua kutulia na kuamua kuwa na familia yake.

Khan amesema kuwa baada ya kufunya sherehe hiyo ya dini ya kiislam iliyofanyika huko Marekani,ametaka marafiki zake wanaoishi Uingereza kukaa tayari kwa pati kubwa itakayofanyika huko wiki ijayo.

1 comment: